Kampuni 3 Zamtaka Mtoto wa Wema:

 

wema seoetu24

Kampuni tatu zimejitokeza kutaka kumtumia kibiashara mtoto atakayezaliwa baada ya staa wa filamu Wema Sepetu kujifungua baadaye mwaka huu.

Chanzo cha uhakika kilicho karibu na staa huyo, kimesema kampuni hizo ambazo hakuzitaja kwa kushindwa kukariri majina yake, zimeshafanya mazungumzo ya awali na Wema, kwani wanaamini mtoto huyo atakuwa kivutio kikubwa.

“Hivi ninavyokuambia licha ya kampuni hizo, tayari wengine wamejitokeza na kudai watamvalisha kwa muda wa mwaka mzima mtoto huyo,” kilisema chanzo hicho.

Gazeti hili lilimtafuta muigizaji huyo na kuulizia juu ya ishu hiyo, ambapo alicheka na kudai hayuko katika nafasi nzuri kwa muda huo ili kuzungumzia suala hilo hadi hapo baadaye.
“Kwa sasa ni mapema mno kuzungumzia hilo jambo, nitaweka wazi baadaye,” alisema Wema

Chanzo: GPL

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

 

Tupe maoni yako hapo Chini..!!

Zari Ahofia Kuishi Bongo! SOMA HAPA SABABU

ZARI8711

Dar es Salaam: Ubuyu! Tumbuatumbua ya majipu ya Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’ inadaiwa kumtisha mwandani wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kuja kuishi Bongo ikidaiwa kisa ni utajiri mkubwa alionao wenye shaka juu ya malipo ya ushuru na mapato.
Habari kutoka kwenye chanzo cha ndani cha familia ya Diamond, zimeeleza kuwa Zari alikuwa na mpango wa kuhamishia miradi na makazi yake rasmi Dar mwanzoni mwa mwaka 2016 lakini ndoto hiyo inaonekana kuyeyuka.
Chanzo hicho kilieleza kuwa, familia ya Diamond imekuwa ikimshinikiza jamaa huyo amshawishi Zari kuwekeza Bongo lakini kwa sasa mpango huo umefutika kwani mwanadada huyo anaogopa kutumbuliwa majip
“Unajua Zari anafuatilia kila kitu kinachoendelea nchini. Kwa hiyo usidhani hajui mambo ya TRA (Mamlaka ya Mapato) yalivyochachamaa.
“Unajua anasema akihamia Bongo itabidi aingize nchini yale magari yake ya kifahari anayotembelea akiwa Sauz (Afrika Kusini) au Uganda lakini anahofia tumbua majipu ya Magufuli.
“Wewe fikiria kama lile Range (Rover) la Wema (Sepetu) limekamatwa na TRA, itashindikana nini kukamata Hummer au Lamborghini ya Zari?
“Nafikiri ishu ni utajiri wake. Nilishasoma kwenye vyombo vya habari vya Uganda kuwa utajiri wake wa ghafla umekuwa ukiibua sana maswali na yeye huwa hapendi kuzungumzia vyanzo vya utajiri wake,” kilinyetisha chanzo chetu.
Baada ya kumwagiwa ubuyu huo, mwanahabari wetu alithibitisha kuwa kweli Zari hayupo Bongo yupo Sauz hivyo alimsaka Diamond ambaye alikuwa na haya ya kusema: “Zari ana miradi mingi, muda wa kuwekeza Bongo ukifika atakuja kufanya hivyo.
uhusu mheshimiwa (Magufuli) mimi nampongeza kwa kutumbua majipu kwa sababu tulikuwa tunahitaji kiongozi kama yeye,” alisema Diamond na kuongeza kuwa mpango wa Zari wa kuja kuishi Dar upo palepale.

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

 

Tupe maoni yako hapo Chini..!!

by :BONGOMOVIE