TUMBO LA JIDE LAZUA MASWALI UKUMBINI

TUMBO LA JIDE LAZUA MASWALI UKUMBINI

13122891_1165800923452777_9083887204878120222_o

Dar es Salaam: Habari njema? Kitumbo cha staa wa Miondoko ya Afro-Pop Bongo, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ au ‘Lady Jaydee’ kimezua minong’ono na maswali ukumbini baada ya kuonekana kama kinaanza kuchomoza.

Wapenda ‘ubuyu’ walisikika wakikisema kitumbo cha Jide mara baada ya kutinga kwenye Ukumbi wa Samaki Samaki, Masaki jijini Dar ambako kulikuwa na uzinduzi wa video mpya ya mwanadada huyo inayokwenda kwa jina la Ndi Ndi Ndi.
Shushushu wetu aliyekuwa ametega ‘mingo’ ukumbini humo, alimshuhudia Jide akisaidiwa kushuka ngazi na mtu maalum ili kusitokee hitilafu huku macho ya wengi yakiwa kwenye tumbo lake.

Maswali hayo yaliongezeka zaidi baada ya Jide kusogea stejini wakati akiitambulisha video hiyo kwa wadau waliohudhuria ambapo kwa muda mrefu aliugandisha mkono wake wa kulia kwenye tumbo lake.

“Jamani mimi nawaambia tumbo la Jide lina neema ndani yake, si unamuona hata mkono haubandui kwenye tumbo, mimi ninahisi mambo yameiva,” alisikika mdada ambaye ndiye aliyeibua minong’ono hiyo ukumbini humo.
Baada ya kumfuata Jide ili kumfikishia ujumbe kuwa tumbo lake limezua maswali na watu wanahisi ana ujauzito, alifunguka:

“Si kweli jamani nikiwa nayo mtajua tu, mimba haijifichi,” alisema Jide ambaye wimbo wake wa Ndi Ndi Ndi ndiyo habari ya mjini kwa sasa kwani unazidi kushika kasi mithili ya moto wa kifuu ndani na nje ya Bongo.

Stori, Risasi Jumamosi

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

 

Tupe maoni yako hapo Chini..!!