Hamisa Mobeto aumbuka APEWA ONYO KALI NA DANUBE

Hamisa Mobeto aumbuka !! Wanasheria wa kampuni ya Danube wadaiwa kumtumia Hamisa barua ya kumtaka afute video ya Zari na Diamond aliyopost wiki chache zilizopita katika akaunt yake. Kwa mujibu wa barua hiyo ambayo imeanza kusambaa Danube wamesema Hamisa sio balozi wa kampuni Yao na wala hawafanyi nae kazi kwahiyo alipost official video ya tangazo la kampuni hiyo kwa manufaa yake binafsi na sio kampuni ambapo katika video hiyo Diamond na Zari wanatangaza bidhaa za kampuni hiyo huku Zari akizungumzia mambo ya hereni. Barua hiyo inaonekana ni ya tarehe 9 October 2017.

Hata hivyo Hamisa tayari amefuta video hiyo ambayo aliipost huku kukiwa na mkorogano mkubwa baada ya habari za kuzaa and Diamond. Haijaeleweka nani amevujisha mitandaoni barua hiyo ambayo mlengwa ni Hamisa kwani wengi walidhani Mobeto alilipwa na kampuni hiyo kupost tangazo hilo

Nini maoni yako ?

Familia Yawakalisha Zari na Mobeto.

DAR ES SALAAM: Warembo waliokuwa kwenye vita ya maneno, Hamisa Mobeto na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamedaiwa kuwekwa kitimoto ili waache kurushiana maneno kwenye mitandao ya kijamii.

Risasi Jumamosi limeelezwa kuwa, kwa nyakati tofauti wawili hao waliwekwa kitimoto na ndugu wa msanii wa Mzazi Mwenzao na kutakiwa waache malumbano hayo mitandaoni kwani hayaleti picha nzuri kwao na ukizingatia kosa limeshafanyika na msanii kukiri hadharani.

“Walichoelezwa tu ni kwamba, waache kutupiana vijembe mitandaoni maana wao sasa hata kama hawatakuwa wake wenza lakini tayari msanii ana damu yake kwa Mobeto. Amekiri kwamba aliteleza na kujikuta ameingia kwenye uhusiano naye hadi kufikia hatua ya kupata mtoto.