Category Archives: europe

kumekucha V.A.D Waja na sehemu ya nne Episode ya nne ya Tamthilia ya MAWENGE ; WASANII WAPYA NDANI

Wale wakali wa filamu na Tamthilia za kiswahili kutoka nchini Denmark waja sasa na sehemu ya nne ya tamthilia yao inayoendelea youtube ya MAWENGE tarehe 06.04.2019 kama kawaida imejaa wasanii maarufu löakini pia sura mpya yaani waSANII WAPYA kabisa tegemea kuwaona toka tamthilia ya mawenge.
Swali tunayo kwa nini roho za YUDA na KAINI uendelea ku tawala na kuongezeka jamani? watu tujifunze kuwa na roho za uruma na tusijipende wenyewe bonyeza link chini kucheki tamthilia hio ya mawenge au waeza watafuta youtube kwa jina la kampuni yao VAD FILM PRODUCTION

walie cheza ni wasani kutoka inchini Danmark kundi la V.A.D the voice of africa in Denmark
Ndani ya EPISOD iyo utakutana naye Lucy Komba, Selembe Toko, Safi Happy, Kay Msabaha, Safari Lukeka, Tatu Musa, Agnes Sakina na wengine wengi



/54279298_435392997202701_9145456304993599488_n.png” alt=”” width=”960″ height=”540″ class=”alignnone size-full wp-image-4779″ />

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX




https://www.youtube.com/watch?v=piL6sseKnBU&t=29s
https://www.youtube.com/watch?v=PfC3NiurMEQ&t=35s

https://www.youtube.com/watch?v=cVF-MJA2LhI&t=24s

BABA KANUMBA AIBUA MAPYA KWA waziri MWAKYEMBE


BABA wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba ameibua mapya kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe baada ya kumwangukia na kumuomba asimsahau katika mikataba aliyosaini mwanaye.

Akizungumza kwa njia ya simu akiwa nyumbani kwake Shinyanga, baba Kanumba alisema anamuomba waziri huyo amsaidie ili aweze kupata haki yake kama mzazi endapo mikataba ya kazi aliyoingia mwanaye enzi za uhai wake itafanikiwa.

Aliendelea kusema kwamba anaiomba serikali iingilie kati suala hilo na endapo fedha hizo za mikataba ya Kanumba zitatoka basi wasaini wote yeye na mama Kanumba na siyo waangalie upande mmoja yaani mama tu.

Namuomba sana Mwakyembe anikumbuke na mimi kwenye kusaini fedha za mikataba ya mwanangu iwapo zitatoka kwani nami nina haki maana nilimlea sana akiwa mdogo mpaka akawa mkubwa nikamuuliza anachagua kukaa wapi ndipo akachagua kwenda kuishi kwa mjomba wake. “Kwa sasa mimi nimekuwa mlemavu wa miguu hivyo naomba na mimi nikumbukwe, na mimi nina haki msinisahau,” alisema baba Kanumba.

Baba Kanumba ameya-zungumza yote hayo ikiwa ni baada ya hivi karibuni Waziri Mwakyembe kuzungumza bungeni kwamba watashughulikia mikataba ya kazi waliyoingia wasanii kama Mzee Majuto na Kanumba ili waweze kupata haki zao

STORI: Gladness Mallya, Risasi Mchanganyiko

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx


https://www.youtube.com/watch?v=rP2QM_PUKqY



https://www.youtube.com/watch?v=Db3LaSev0BY