SHEHE Amcharukia Jackline Wolper. Ni kutokana na tabia yake ya kubadili badili dini.

 

 

SHEHE Amcharukia Jackline Wolper. Ni kutokana na tabia yake ya kubadili badili dini.

TABIA ya staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kubadilibadili dini mara kwa mara imeonekana kuwakera watu mbalimbali akiwemo Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum ambaye amemcharukia vikali.

Wolper kiimani ni Mkristo lakini hivi karibuni alibadili na kuwa Muislam kabla ya kurejea tena kwenye imani yake ya awali ya ukristo.

Sababu ya Wolper kubadili dini ilikuwa ni kufunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake Abdallah Mtoro ‘Dalas’, walipoachana akaamua kurudi kwenye ukristo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi juzikati, Shehe Salum, alisema Wolper anapaswa kujichunguza na kubadilika haraka kwani kitendo anachofanya ni kinyume na taratibu za dini.
“Siyo vizuri hata kidogo na hata dini zote zinakemea kitendo cha kuchezeachezea dini kwani ni chukizo kwa Mungu.

“Kwa upande wa Dini ya Kiislamu, kuna sheria kali zaidi kwa mtu akionekana na tabia hiyo, anaweza hata kuuawa hivyo wanaofanya mchezo huo waache kwani siyo vizuri. Huko ni kumfanyia Mungu dhihaka,” alisema Shehe Salum na kuongeza:

“Unajua suala la imani ni kitu kinachomhusu mtu binafsi, ni vyema kufanya uamuzi wa hakika na kushika njia moja na siyo kufanya dhihaka na dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kitu kibaya sana.”
Naye Juma Suleiman, mkazi wa Ilala, jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wetu kuwa, katika imani ya kiislam kunakatazwa watu kucheza na dini huku akisisitiza anayefanya hivyo anaweza kulaaniwa.