Natafuta mtu mwenye kipaji cha kuongea: Rehema Nkalami

JINA KAMILI UNAITWA NANI
Naitwa Rehema Amiry Nkalami natokea Tanga Tanzania .Ila naishi silkeborg Denmark  ni mtangazaji wa swahili talk radio.

http://www.shoutcast.com/Internet-Radio/swahili%20talk%20radio

401299_168329066660613_904520870_nRehema Nkalami akiwa Studio

Hongera sana kwa kazi yako nzuri ya utangazaji, sasa ningependa kufahamu hii kazi ulianza lini
Asante sana , hii kazi ya utangazaji niliianza mwaka 2012  . sifanyi hii kazi sababu  napenda utangazaji tu ,hapana bali napenda kuutangaza Uafrika pamoja na lengo la kukuza lugha za kiswahili na utamaduni wa mwafrika ulaya na nchi zote ulimwenguni.

1374284_222645964562256_317310790_n

Rehema akiwa na kikundi cha African Umoja Denmark kwenye sherehe ya utamaduni

577440_227389214087931_2133106632_nRehema akitangaza mavazi ya kiafrica kwenye Swahili talk radio

Unaweza vipi kufanya hii kazi ukizingatia wewe upo ugenini
Siku zote mtu anayenitia nguvu ni mme wangu mpendwa Søren . Yeye ni muandishi wa habari pia ni mtangazaji wa denish radio station,
lakini pia mimi nina studio yangu hapa silkeborg na zaidi nafanya kazi na jamii ya waafrica, pia watu wote ambao wanapenda kuongelea mambo yanayohusu Africa wanakaribishwa studio.

577577_170101323150054_825325804_nRehema akiwa studio na Leonidas  kwenye kipindi cha biblia1471962_241447069348812_1335462501_nRehema akimuhoji Mr Nice mwanamziki  kutoka Tanzania

Hongera sana kwa kazi zako nzuri, sasa ningependa kujua mipango yako ya baadae.
Mipango yangu ni kuanzisha Tv talk show ambayo itaitwa REHEMA SHOW na kwa sasa maandalizi yote yameshakamilika  ,niko kwenye hatua za mwisho ili kuanza kazi hiyo, na sababu mimi nitakuwa busy na talk show hivyo natafuta msaidizi kwenye radio mwezi wa pili ,mtu mwenye kipaji cha kuongea hasa kipindi cha kuchekesha

1482156_10202894906313386_1034128203_nRehema akiwa na Lucy Komba muigizaji toka Tanzania

1472036_241447519348767_989828999_n

Rehema akimuoji Raisi wa v.a.d film production Mr Safari Lukeka

Hongera sana dada Rehema kwa kazi nzuri unazozifanya ikiwa si tu kwa utangazaji bali hata kuutangaza uafrika pia kushughulika na mambo yanayousu jamii ya waafrica , Swahili movies inakupongeza na kushukuru kwa ushirikiano wako .

Usisahau kulike and share faceboook page yetu swahili movies .com