Actor Abou Hermis Twaleeb Covers MOVIE STAR MAGAZINE With Advice for his fellow actors

Muigizaji  Abou Hermis Twaleeb amekava katika gazeti jipya la Movie Star ambalo litakuwa linakujia kila wiki na kitendo hiki kimekuja baada ya mashindano yaliyokuwa yanafanyika katika kinyanganyilo cha kumtafuta mkali wa kuigiza kati ya Abou Hermis  Twaleeb na Muigizaji mwenzake Bjohn Mausa lakini kula za mashabiki zikampendekeza Abou Hermis Twaleeb ….. na kwa siku za baadae kava hili lina mpango wa kuanza kuchapishwa na kusambazwa hivyo wapenzi wa habari  za swahili movies Diaspora mkae mkao wa kula

10805532_590300521115157_1963510206_n

kushoto Abou Hermis Twaleeb  kulia ni   BJohn Mausa

Hii ndio kazi ya B JOHN MAUSA  RIZIKI YA MNYONGE

Hii ndio kazi ya Abou  Twaleeb  AFRICAN BOY

10805020_591880304290512_2061131089_n

HUU NDIO USHAURI ALIOTOWA KWA WAIGIZAJI WENZAKE BNAADA YA KUSHINDA ABOU

HERMIS TWALEEB

Ushauri wangu mkubwa kwa wasanii chipukizi (kama mimi) ni kuwa seriously na kazi zao pale wanapopata nafasi za kufanya hivyo, wasifanye kazi kwa ajili tu ya kujulikana na kupata majina makubwa…wafanye kazi nzuri,kwa bidii na kwa kujituma sana ili waendelee zaidi kiusanii.
1781150_1513538822236176_3874772989698779938_o
PILI:  ni UMOJA…wawe na ushirikiane na wasanii wenzao bila kujali NANI ZAIDI. Umoja ni silaha kubwa ya kujifunza mengi kwa kuwa kila binaadamu anacho ana mtazamo wake, mawazo yetu yako tofauti sana, na kama vile ambavyo mkubwa anaweza kumuongoza mdogo..basi mdogo nae aamini kuwa anao uwezo wa kumuongoza mkubwa ikiwa tu Umoja, Upendo, Busara na Heshima vitatawala kati yao na hapo MAENDELEO YATAPATIKANA….
La mwisho ningependa kuwashauri wasanii wote chipukizi WASIKATISHWE TAMAA kwa namna yeyote ile. Safari ya kuwa msanii ni ngumu sana na ina mitihani mingi sana ambayo inakutegemea wewe mwenyewe utapambana nayo vipi. Unaweza kufuatwa-fuatwa, kutukanwa, kudharauliwa, kusingiziwa mabaya, kuonekana haujuwi chochote, na hata wakati mwingine ukatamani ujitoe na kufuta ndoto zako kiusanii…Hakuna kilicho rahisi katika FANI yoyote na wengi wanakata tamaa kwa kufuata nani anasema nini na nami anataka nifanye nini..wewe jiamini na upiganie kile unachotaka wewe na siyo wanachotaka wengine kwa kuwa UKIFANIKIWA ni faida yako mwenyewe na wengine..hivyo wasanii chipukizi MSITATE TAMAA DAIMA….MUNGU ATAWAONGOZA..
Mwisho alimalizia kwa kuwashukuru mashabiki wake wote waliompigia kura na kusema kwa kufanya hivyo wameonyesha upendo na ushirikiano .

 

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

CREDIT :Here

POSTED BY : Hamm Chande

Tupe maoni yako hapo Chini..!!