Category Archives: africa

STEVE NYERERE AMUONYA WEMA SEPETU

Stori: Shani Ramadhani

MWENYEKITI wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Stive Nyerere’ ameibuka na kumuonya Wema Sepetu kupiga kazi na kuepuka umaarufu bila kazi.

wem
Steve na Wema Sepetu

Nyerere amemtaka Wema aachane na skendo za kila kukicha kwani hazina maana kama kazi ya sanaa aliyoichagua kama njia ya kumuingizia kipato.

STEVENYERERE531
Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Stive Nyerere’.

Nyerere amemtaka Wema aachane na skendo za kila kukicha kwani hazina maana kama kazi ya sanaa aliyoichagua kama njia ya kumuingizia kipato.

4X7A9552
Wema Sepetu akiwa na Diamond Platinum.

“Kwanza nampongeza sana Diamond kwa tuzo zote alizopata kwa kuwa alistahili lakini Wema naye anapaswa kuiga mfano, vinginevyo atakuwa maarufu bila ya heshima,” alisema Steve Nyerere.

CREDIT: global publisher

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

Ndoa ya Ustazi Juma na Johari yanukia. Asema Johari atakuwa mke wake wa pili

bbbnJohari na Ostadh Juma na Musoma

PENZI limekolea na kinachoonekana sasa kwa Ostaz Juma Namusoma ni kukazia penzi lake kwa mwanadada Blandina Chagula ‘Johari’ anayesumbua kwenye Bongo movies.

 

Kwa mujibu wa mtandao wa GPL zinasema kwamba Ostaz alifunga safari kwenda nchini Afrika Kusini kwa mapumziko mafupi lakini pia kumnunulia mpenzi wake huyo zawadi mbalimbali kwa lengo la kupalilia uchumba wao.

“Jamaa alikuwa Sauzi (Afika Kusini), aliondoka hapa tarehe 17 (Machi) na amerudi tarehe 21. Kamletea zawadi kibao lakini kubwa zaidi ni kamera kubwa, nzuri ya kisasa kwa ajili ya kerekodia filamu,” kilipasha chanzo hicho.

GPL ilifanikiwa kumpata Ostaz kwa njia ya simu, akafafanua: “Ni kweli nilikuwa Afrika Kusini. Kuhusu Johari, ni kweli si mke wangu? Nimemletea zawadi nyingi sana, achana na hiyo kamera unayosema.

“Lengo ni kuweka uchumba wangu  na yeye sawa. Nilitamani sana kusafiri naye lakini sikutaka kufanya hivyo ili kuweka usawa, mke wangu asione nimeegemea zaidi kwa mke mdogo.”

Alipoulizwa kwa nini amemuita Johari mkewe, haraka alisema: “Ndoa ipo karibu, nimeshaamua Johari awe mke wangu wa pili. Wadau wasubiri waone, uzuri ni kwamba dini yangu si kikwazo.”

CREDIT: BONGO MOVIES

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more