Category Archives: fun

Actress Devotha Alfred Alikacha shavu la modeling (akataa kazi ya modeling)Na kuingia kwenye utangazaji

Muigizaji Mrembo na chipukizi aamua kulikacha shavu la modeling kwenye kampuni kubwa ya kijerumani na kuingia  kwenye utangazaji. Mrembo huyo mwenye mashiko na aliye serious na kazi yake ya uigizaji tulipomuhoji kuusiana na sababu gani za kuukacha uanamitindo ilihali yeye ni msanii na ana sifa zote za kufanya  vizuri kwenye fani hiyo ya mitindo alikuwa na haya ya kusema.

1506576_613726242049828_1216904425_n

Actress and TV host Devotha Alfred

Ni kweli nilipata kazi ya kufanya modeling kwenye kampuni kubwa hapa ujerumani inayofanya kazi na wanamitindo wa kiafrica , lakini nilikataa kuingia kwenye fani hiyo kwa sababu zangu binafsi ,ila kubwa kabisa ni muda kwa sasa nina programu nyingi ambazo zote zinaniitaji mimi niivest muda mwingi kuzishughulikia ikiwa kwa sasa nimechukuliwa na kampuni ya Afrowood ambayo ninawafanyia television show kwa lugha ya kiswahili japo show ina jina langu  yaani DEVOTHA SHOW,

Lakini pia kwenye mambo yangu ya filamu mimi bado mchanga sana hivyo bado nina kazi kubwa ya kufanya kuinua sanaa yangu ikiwa pamoja na kuitangaza zaidi, kwa kufanya kazi nyingi nzuri na za kimataifa ,lengo langu kubwa ni kufanya kazi zenye ubora

Pia mimi ni mwanafunzi hapa ujerumani hivyo pamoja na shughui zangu zote za kilasiku bado shule inaniitaji nifanye vizuri ili nifikie malengo yangu, sasa najikuta muda wangu mwingi uko covered sina mda wa ziada wa kuingia kwenye mitindo kwani mitindo nayo ni kazi inayoitaji muda na kujitoa , ila kwa waafrica wanaoishi ulaya na hasa germany , kama wanajua wana vigezo vya kufanya kazi hiyo kimataifa basi hapo chini nitaweka contact ya hiyo kampuni ili mrembo ambaye yuko interested atawasilina nao wajue watamsaidia vipi kutimiza ndoto zake .

10011583_1385426591737192_622802589156509862_oactress devotha on pose

IMG_6987devotha ready for tv host

10155687_635105009878436_1948487968820611711_nTulipouliza devotha kuwa hizo ndio sababu za kukataa kazi hiyo hiyo kwa sababu za kimaadili au mavazi alikuwa na haya ya kusema

“hhahhahhahah  kiasi  sana  si kweli sana kuwa nimekataa kwa sababu ya maadili maana  kila kazi ina maadili yake na naheshimu kazi hii ya mitindo kwani kuna watu wanafanyakazi hii na bado wana image nzuri kwenye jamiii, ila kwa mimi tayari ni mtangazaji sasa tayari nimeshafunikwa na maadili mengine hivyo kuniwia ugumu sana kuingia kwenye mitindo kwani itaniweka kwenye sehemu ambayo mashabiki na jamii itashindwa sana kunielewa nasimamia wapi nafikiri hizi kazi mbili nilizonazo zinatosha kwa sasa asante.

https://www.youtube.com/watch?v=LoBEoYLTxuo

BONYEZA HAPA KUOMBA KAZI YA MODELING GERMANY

http://www.afrikanische-models.de/

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more