Mwanamziki Mtanzania anayeishi Denmark Geofrey McLaughlin Ametoa wito kuomba watanzania na waafrika wote wanaoishi nje ya nchi zao wajitaidi kwa hali na mali kusaidia watoto wenye hali ngumu kimaisha ,
yaani watoto yatima na watoto wa Mitaani , Geofrey ameongea hayo baada ya kutua nchini Tanzania wiki iliyopita na kubahatika kuona idadi ya watoto wa mitaani na yatima imeongezeka na wako wanadhulula kila sehemu hali imemsikitisha ukizingatia watoto hao wako kwenye mazingira magumu sana .na kusema kuandika h aya katika mtandao mmoja wa kijamii ikiwa ameweka na hizo picha
Ninaomba Mungu anisaidie na kunifanikisha kazi zangu , singida ni Mji wangu Tanzania ni nchi yangu , Africa ni bala langu na hawa ni watoto wetu sote tuwapende na tuwakumbuke kwa chochote ili Mungu aendelee kutubaliki .
Msanii Geofrey McLaughlin akiwa na baadhi ya watoto hao
Hakika Hiki ni kitengo cha Ubinaadamu , kukumbushana kusaidia wenye uhitaji .Swahili movies inampongeza msanii huyu alietambulishwa na kibao cha The black Nilivyokupenda Remix na kumtakia Holyday Njema Africa .
Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more
CREDIT :here
Tupe maoni yako hapo Chini..!!