Katika kipindi cha kuelekea siku kuu ya Pasaka au christmass, ni jambo la kawaida kukuta nyumba za waumini wa dini ya Kikristo zikiwa zimepambwa na picha mbalimbali za Yesu, lakini pia kama wewe ni muumini wa dini hiyo, unapotajiwa au kulisikia jina la Yesu, kuna picha fulani inakujia mawazoni, kuna sura fulani inakujia mawazoni, si picha au sura nyingine, bali ni sura ya Yesu.
Wapo wanaodhani kuwa picha hiyo au sura hiyo ndiyo Yesu mwenyewe aliyezaliwa yapata miaka 2000 iliyopita, hapana, hakuna anayejua sura ya Yesu ikoje, anaonekana vipi, bali mtu huyo ambaye ulimwengu umezoea kumwona kama ndiyo Yesu wa Nazareti, huyu ni jamaa mmoja anayejulikana kwa jina la Brian Deacon, huyu ndiyo jamaa aliyeigiza ile filamu maarufu ya Yesu, inayojulikana kwa jina la ‘Jesus Film’ mwaka 1979. filamu hiyo iliigizwa na watu mbalimbali ambao wengine wapo hai mpaka leo, picha za filamu hiyo zilipigwa nchini Israeli.
Je Brian Deacon ni nani?
Brian Deacon ndio jina halisi la mwigizaji huyo ambaye ni raia wa Uingereza alizaliwa tarehe 13/02/1949 huko Oxford nchini Uingereza ni mtoto wa pili katika familia yao, baba yake alikuwa ni fundi makenika huku mama yake akiwa akiwa ni Muuguzi.
Filamu
Alipata nafasi ya kuigiza filamu ya Yesu baada ya kupita mchujo, katika mchujo huo walijitokeza waigizaji zaidi ya 1000. Brian Deacon aliwahi kunukuliwa akisema kuwa, filamu hiyo ya Yesu ilimfanya yeye kuokoka baada ya kuitamaza kwani kabla ya kuigiza filamu hiyo hakuwa ameokoka. ilichukua miezi saba Mpaka filamu hiyo inakamilika
Filamu nyingine alizowai kucheza ni kama A Zed & Two ( 1985), Vampyres ( 1974 ), The Triple Echo ( 1972) , Lillie (1978)SOURCE : venancefuraha.blogspot
Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more
Tupe maoni yako hapo Chini..!!
Imeandaliwa na Furaha Venance, Habari na picha kwa msaada wa Mtandao