Rizos Babingwa ambaye ni meneja pia ni muigizaji wa kundi la V.A.D nchini Denmark kundi linalofanya vizuri kwenye filamu za kiswahili , amepewa kikombe cha heshima kutoka kampuni kubwa ya filamu ya Scandinavia inayojulikana kwa Nordisk Film kwa kukfanikisha kukuza filamu za kiswahili nchini scandinavia na ulaya kwa ujumla ,
Meneja huyo anayejitahidi kualika na kukaribisha mastar mbalimbali kufanya nao kazi kama Lucy Komba kutoka Tanzania ambaye walifanya nae Filamu ya Tanzania to Denmark , kama haitoshi meneja huyo alifanikisha kuja kwa mkongwe wa muziki Mr nice na kufanikiwa kufanya nae Film inayoitwa NIMUAMINI NANI na ndipo kuonyesha kukubali na kutambua juhudi zake kampuni ya kidenish imempa kikombe ambacho kina jina lake angalia hapo chini.
Meneja na Muigizaji Rizos Babingwa
Meneja na Muigizaji Rizos Babingwaakiwa na Mr nice
Meneja na Muigizaji Rizos Babingwaakiwa naLucy Komba
Kikombe cha heshima alichopewa Rizos Babingwa kuinua filamu za kiswahili ulaya