SIFANYI FILM KUTAKA UMAARUFU AU USHINDANI: Sallai majasiri

Kutana na  Sallai majasiri ni mkongomani  mswahili ambaye anaishi Holland ameoa na ana  watoto  watatu ni mwigizaji lakini pia ni mmiliki wa sallai majasiri  Pro.  baada ya swahili movies kuona kazi zake za film nzuri anazofanya hasa movie za gospel ndipo ilipoamua kujua machache kuusu huduma yake hii anayotoa ya film na mipango yake  tuendelee……

1476032_680949748602583_1851307394_n

Sallai majasiri

Hongera ulianza lini kazi ya filamu  Na nini kilikusukuma?

Mama yangu ni chachu kubwa sana mimi kua na msukumo wa kuigiza ,maana hata yeye nimuigizaji kanisani hata sasa. Tangu nikiwa mdogo niliigiza kanisani kwenye vipindi vya sunday school.

Waooh that is amazing hongeraSasa niambie unaigiza bado kanisani tu au unafanya film pia ?

Vyote na vifanya .kanisani naigiza na film naigiza. Hadi sasa nimesha shiriki filamu tatu ya kwanza kabisa niliigizia Kenya chini ya UNHCR ;  Sugar mamy  2010 ya pili niliishirikiana na rafiki zangu hapa Holland  UMDHANIAE NDIE KUMBE SIYE na ya tatu ni filamu yangu nilioiandika mwenyewe nikishirikiana na mdogo wangu mpendwa Gilbert .  kwa jina la MWANZO WA MWISHO.

1508340_679983655365859_1814581125_nJarno Feenstra , Sandrine , Solange location

 Sasa wewe unafanya gospel film na kwenye film kuna vikwazo vingi kuanzia mavazi na uhusika unakabiliana vipi ikiwa wewe umeokoka hasa love scene?

Mimi sishiriki katika kila movie , haswaa zisizokua na maadili ya kuijenga jamii.
nimejiwekea utaratibu huo , maana nia yangu siyo umaarufu bali kupeleka injili ya YESU kupitia filamu,
1476869_679983622032529_620106517_n                                      Sallai majasiri na  Sandrine Rugohe wakiwa location
1079442_679983642032527_1189743750_n
                                                            Kuba na Blandine wakiwa location

 Watu wanapokea vipi swala la wewe au mtu alieokoka kufanya film kwa ujumla

Wengi kwa sasa maana ndiyo mwanzo ,  wanakutia moyo kisha wanakuvunja moyo wengine wanadhani tu unacheza mchezo wa muda tu . wengine wanasimama na sisi kwa hali na mali.  Kazi zinapokelewa tofauti taofauti , shetani anafanya  kazi kwa hali ya juu kwa sasa , ndiyo maana kazi kama za injili zinaweza kuonekana kama tu kupoteza wakati. shetani anapambana lakini MUNGU anashinda !!!

1470458_679983625365862_861989377_nSallai ,Gilbert na Jarno Feenstra wakiwa location

Ila nafarijika sana maana napokea simu na ujumbe wa email kutoka maeneo mbali mbali ya dunia , kunipongeza nakunitia moyo kwa filamu ya MWANZO WA MWISHO haswa watu wazima wanafurahia sana , maana ni filamu unazoweka kuangalia ukiwa na familia nzima , bila kupatwa na aibu ya kuona yanayoendelea katika filamu hiyo

shabaa yangu nikumpelekea YESU KRISTO nafsi nyingi zaidi  .Naitaji maombi yenu sana

1529669_679983652032526_1000948412_o Kushoto ni Sandrine Rugohe,Sallai ,Sandrine prince na aliyeshika camera kate

 kwa sasa kuna kazi yoyote inakuja au Bado mwanzo na mwisho na  itatoka lini Watu wakae mkao wa kula

bado ni mapema sana kusema hilo , lakini movie yangu ya MWANZO MWISHO itapatikana Youtube , kama nilivyo ahidi. Najiandaa sasa kuja na filamu mpya itakayo leta na kufungua ukurasa mpya wa filamu hapa Ulaya na kote kwa ujumla  JIPU KANISANI.  nitakayo shirikiana na watu ninaowaeshimu na kupenda kazi zao kama , Devotha  Alferd , Selembe Toko , Gilbert Fataki , Ashley Toto, Joy Simgala , Rosette Sallai , Esther Fataki ,Jarno Feenstra , Blandine Wakengo , Antoinette K, Guilaine. Majina ni mengi mno nikiyataja na wote ni wenye  vipaji na wasio bahatisha…

Una mipango gani  ya baadae ,watu wategemee nini  ?

Ni vibaya sana kutangaza mipango ya baadae maana kama ukiwa vitani , adui ni ibilisi , Lakini kwa uweza wa MUNGU muumba watu wakubwa kwa watoto wafurahie maana kila ,Mungu atakapo nijalia kutoa filamu , itawabadilisha maishani mwao , haitowaacha kubaki kama awali , watarajie Mungu kusema nao kupitia mimi na wote ninaoshirikiana nao , akiwamo mke wangu , na kaka yangu   Gilbert pamoja na marafiki na wapendwa wengi.

1492893_679983612032530_698881611_nSandrine na Gilbert wakiwa location

http://www.youtube.com/watch?v=dHwyAXASqus

Nimepata tena nafasi ya kwenda kushiriki filamu ya UN hapa hapa Ulaya .na Napenda kuwashukuru wote walioziacha shughuli zao na kuja kuniunga mkono ku hakikisha filamu ya  Mwanzo wa mwisho inasimama Sandrine Rugohe ,  Blandine Wakengo  Antoinette  Rossi,Solange  Jacqueline , na Betty Zelalem , Sandrine Prince ,Jarno Feenstra, Gabby Kihota ,Solange Nyarwka  ,Director Kate ,  Gilbert Fataki   na wengine ambao labda sijawataja maana niwengi mno .  MUCH LOVE

Swahili movies  inashukuru sana Sallai majasiri  kwa ushirikiano wako.tunakutakia kazi njema

Usisahau kulike and share pia unatupata facebook .  swahili movies .com
pia follow us instagram  swahilimovies