mfahamu msaniii mrembo aliyeanzia kuigiza kanisani

mimi jina langu ni bethlehem zelalem mu Ethiopia mzaliwa kenya naongea lugha 3 English kiswahili na lugha ya wazazi na pia lugha ya ki holland

  1538668_479941288774504_8167883335420772445_nActress Beth zelalem

mimi mtoto wa kwanza kwetu,nimekuja na wazazi baba na mama hapa Holland,niko na two brothers but mimi naishi kivyangu sipo na wazazi mimi nimeolewa na jina kamili ya mume wangu ni Alex Bikorimana ambaye ni president wa group cha ngg production

10152425_479945632107403_5651200361613554220_nActress Beth zelalem na familia yake

nimeanza kuigiza in summer time 2012 movie ya kwanza iko kwenye youtube umdhaniae kumbe sie

1529901_656770124364352_1709377694_o

 

kuna movie ambayo nilimsaidia Sallai majasiri njoo ya kwanza but I don’t no kama imesha toka that’s why  nasema ” umudhaniae kumbe sie ” niyakwanza sababu  imesha toka

Nilianza kucheza kwanza kanisani vitu mimi nilianzia kwa theater ya kanisa kucheza mbele ta watunikitu napenda sana njoo sababu mimi niko kwa film

SONY DSCActress Beth zelalem behind the scene   ndai ya filamu yao mpya

kundi ya ngg-production.com ni kundi ipo nchini Holland haina ubaguzi kila kabila tofauti zinakaribishwa .

kwasababu kuwa ngg production ni kundi ambalo tunapenda kufunza jamii yakisasa na pia kuelimisha watu tutakuwa na uzinduzi ya why facebook on 0 2-05-2014  yani hivi tuko kwene maandalizi.

SONY DSCActress Beth zelalem  Alex , na Blandine Wakengo behind the scene   ndani ya filamu yao mpya

Busy na kuandaa program vile itakuwa na mimi niko moja wa viongozi mimi ni mtu napenda sasa heshima kama mke au mtu nimeolewa

ndio nivingumu saa moja kusema tunamuitaji flani kutoka ngg group aje atu help nisawa kabisa ila ukifwata mtu muhusika

coz tunafatwa kazi zetu very well zaidi nitaongeza wasanii tuwache wivu na chuki kwa kazi ya wenzetu magazeti eti flani amesema hivi haipendezi  itakuwa tunafunza kuigiza movie ao kuigiza wivu? ?

so tupendane tuwe na umoja na tu support each other kwa kazi hatutafika mbali bila upendo na umoja

10153044_479945608774072_1415436425705943495_n

mwisho mimi napenda sana ndoa yangu na niko very happy with my life sikosi kitu ndoa ninayo kugaramiwa ninagaramia kama mke anapashwa kuwa

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

 

 

 

 

 

 

 

Wema Sepetu azua Timbwili zito kutokana na kuandikwa skendo mbovu kila siku

Star wa filamu nchini Wema Sepetu amezua timbwili la kufa mtu katika ofisi za magazeti ya Globalpublishers juzi Jumatatu kwa madai kuwa magazeti hayo yamekuwa yakimuandika vibaya yeye pamoja na mpenzi wake Diamond Platinumz. Wema alitinga katika ofisi hizo na baadhi ya wapambe na wafanyakazi wa kampuni yake akiwemo meneja wake Martin Kadinda na Petit Man Wakuache, Wema alitinga katika ofisi hizo huku akiwa ameshikilia gazeti la Ijumaa Wikienda la siku hiyo lililokuwa na kichwa cha habari “Diamond Atamani Ushoga!” habari ambayo watu wengi mitandaoni waliipinga kuwa mwandishi wa habari hiyo alikurupuka kwa madai Diamond alichukua wigi la Wema na kulivaa kwa utani kama mpenzi wake. Vile vile Wema Sepetu alichukia kwa habari ilizoandikwa kuwa yeye na Aunty Ezekiel wanaashiria vitendo vya kisagaji kufuatia picha zao kutumika katika moja ya magazeti hayo kuwa walibusiana kitu ambacho Wema alisema katika habari hiyo kupigana mabusu kwao ni jambo la kawaida sana na sio kama ilivyoandikwa.
Habari nzima iliyoandikwa na Globalpublishers katika gazeti la leo ni hii hapa chini

Stori: Sifael Paul
HOVYOOO! Wema Isaac Sepetu aliye pia Miss Tanzania 2006, amejitoa fahamu kwa kupandisha mzuka na kutinga makao makuu ya Kampuni ya Global Publishers, Bamaga-Mwenge, Dar na kuzua timbwili la aina yake kisa kikiwa ni kuandikwa kwa habari zake na mpenziwe, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’

WEMASEPETA_GLOBALNEWSROOM8

Wema akiwa ndani ya ofisi za Global na sura ya ‘kuua mtu’, mkononi akiwa na gazeti la Ijumaa Wikienda lenye stori: DIAMOND ATAMANI USHOGA. Kushoto ni mpambe na mfanyakazi wake Petit Man Wakuache. Tukio hilo la kumchoresha staa huyo mwenye vituko kila kukicha, lilijiri Jumatatu iliyopita kwenye ofisi za Global ambao ni wachapishaji wa gazeti hili (Amani), Uwazi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Championi na Risasi majira ya mchana kweupe hivyo kufunga mtaa huku wapita njia wakimzodoa kwa maneno ya kejeli.

ATINGA NA WAPAMBE DHAIFU
Akiwa na kundi la wapambe dhaifu na goigoi wakiongozwa na meneja wake, Martin Kadinda waliosimama nje ya ofisi hizo, Wema alifika kwa upole akionekana mkarimu kwa mlinzi ambapo aliomba kuonana na mwandishi nguli wa magazeti pendwa, Imelda Mtema.

Mlinzi alimruhusu kwa vile Global ni mjengo wa mastaa na watu wasio mastaa, huwa hawakauki kuingia na kutoka kwa mambo mbalimbali.
Wema alipofika mapokezi, pia aliomba kuonana na mwandishi huyo lakini tofauti na utaratibu ambapo huwa mgeni akifika huulizwa kama ana ‘apointimenti’ ili aitiwe anayemhitaji, Wema alipitiliza kwa nguvu hadi chumba cha habari akifuatana na kijana aliyekuwa akimrekodi.

 

WEMASEPETA_GLOBALNEWSROOM18 WEMASEPETA_GLOBALNEWSROOM19

Akiwa ndani ya chumba cha habari, Wema aliuliza kwa sauti ya juu na ya kujiamini: “Imelda yupo wapi? Nauliza Imelda yupo wapi?”

WEMA NA IMELDA
Katika kumtafuta Imelda kwa macho kwa sababu chumba cha habari ni kikubwa huku akionywa na wahariri kwamba atulize mzuka kisha aeleze shida yake, Wema alimuona Imelda akitoa maelezo kwa Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa ya Global, Oscar Ndauka kuhusu habari aliyokuwa ameifuatilia.
Cha kushangaza, Wema alimfuata Imelda mpaka kwenye meza ya mhariri huyo kisha kuanza kufoka kwa sauti ya juu.

MSIKIENI WENYEWE
“Kwa nini mnafuatilia maisha yangu? Kila siku mnaniandika na Diamond. Kwa nini Imelda unaniandika kuwa mimi msagaji?

ATULIZWA, AGOMA
Katika kuhoji huko, mhariri kiongozi alijaribu kumtuliza Wema ambaye alikuwa kama amewehuka: ”‘Wema tuelewane, eleza shida yako kwa utaratibu kwani hakuna ofisi isiyokuwa na utaratibu.”

Pamoja na kuambiwa hivyo bado Wema aliyekuwa ameshika Gazeti la Ijumaa Wikienda toleo la Jumatatu iliyopita, aliendelea kumng’ang’ania Imelda ambaye alikuwa akijaribu kumtuliza:
“Wema twende tukakae pale kwenye meza ya mkutano uwaeleze viongozi wangu tatizo lako. Hiyo stori kuwa wewe ni msagaji mbona haipo, ni gazeti gani?”

WEMASEPETA_GLOBALNEWSROOM17

Licha ya kupewa mwongozo huo, Wema aliendelea kufoka:
“Hivi mnajua mimi ni chizi? Kwa taarifa yenu mimi ni chizi zaidi ya machizi wote, ohooo!”MLINZI ATONYWA, ATIA TIMU
Baada ya hali kuwa tete, mlinzi wa geti kuu alipigiwa simu ya mezani na kujulishwa juu ya Wema kusababisha kazi kusimama ambapo alifika haraka tayari kwa kumtoa nje kwa hiyari yake au lazima.

Ndipo kukatokea timbwili kubwa, wapambe wake ‘goigoi’ nao waliingia wakitaka kufanya vurugu ili kumteka mwandishi huyo lakini kikosi imara cha Global kikiongozwa na Mhariri Kiongozi wa Magazeti ya Championi, Saleh Ally kilijiimarisha na kutuliza fujo hizo huku kikiwa makini kuhakikisha Wema na timu yake hawajeruhiwi hata kidogo.
WEMA ATUMIA GAZETI KAMA SILAHA
Katika purukushani hiyo, Wema alionesha udhaifu wa kumudu varangati pale alipotumia gazeti aliloshika kumpiga nalo mwandishi Imelda, jambo lililodhibitiwa kama Waasi wa M23 wa Kongo walivyodhibitiwa na Majeshi ya Umoja wa Mataifa, akatolewa nje.
MBALI NA WEMA
Ukiachia mbali Wema kutulizwa kwa kutolewa nje kwa nguvu, vijana wake walegevu nao waliwekwa chini ya himaya ya Global kwa kunyang’anywa  kamera ya video iliyokuwa ikitumika kuchukua matukio huku nao wakipigwa picha za kutosha na wapiga picha wetu.
VITA KUBWA, WEMA AVUA VIATU
Nje ya ofisi, ‘vita’ kubwa kati ya Wema na walinzi wa Global (alifika mwingine kutoka lindo la mbali) ilizuka ambapo staa huyo alivua vile viatu vyake virefu vya rangi ya bluu bahari na kuanza kumpiga navyo mmoja wa walinzi hao akiamini anamkomesha lakini pia akadhibitiwa!
9
Wema akiwa anarandaranda kwenye geti kuu akiwa peku, alidondosha matusi ya nguoni ambayo hayaandikiki gazetini kwa namna yalivyokuwa makali. Ilikuwa si rahisi kuamini kuwa yeye ni kioo cha jamii.
Timbwili la Wema na wapambe wake akiwemo Petit Man, ambao hawakufua dafu kwa walinzi na vijana wa Global nje ya ofisi hizo, lilichukua zaidi ya nusu saa huku likikusanya kadamnasi na kusababisha mtaa kujifunga wenyewe.
gf
APEWA KAMERA, KADI NOOOO!
Baadaye Wema aliomba kupewa kamera yake ambapo zoezi hilo lilifanyika lakini ‘memori kadi’ yenye picha walizoanza kurekodi, ilitolewa ili kupisha maridhiano kwanza. Waliambiwa kadi hiyo ilitolewa kwa sababu walirekodi bila idhini au kibali cha Kampuni ya Global.
WEMA AGOMA KUONDOKA
Baada ya kugundua kadi ya kamera ipo chini ya ulinzi wa Global, Wema alitaka kulianzisha tena akidai hawezi kuondoka hadi apewe kadi hiyo lakini uongozi uliweka ngumu. Baadaye aliondoka kimyakimya. Wakati huo wapambe wake walishaondoka kitambo.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, kadi ya kamera hiyo bado ilikuwa inashikiliwa na uongozi wa Global ili kumthibitishia Wema kuwa hawezi kufanya umafia wowote dhidi ya waandishi wa kampuni hiyo yenye nguvu kihabari nchini Tanzania.
WEMASEPETA_GLOBALNEWSROOM5
CREDIT:SWAHILIWORLDPLANET
Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more