Nashukuru Mungu nimenusulika kuuawa na vibaka zaidi ya kumi

1005038_1401851853386966_836153964_n

Msanii wa Jumba arts group Basupa Omari anusurika kuuawa jana jumamosi na Zaidi ya  vibaka   kumi ambao walimvaa bila kujua na kumshambulia ,licha ya kumuumiza vibaya pia wamemuibia pesa na simu katika maeneo ya  mwananyamala Koma koma Dar es salaam TANZANIA. 1008217_1417097995195685_550506328_o                                                Basupa Mvungi

1077253_1417099121862239_980949299_oBasupa Mvungi

Baada ya matibabu ya haraka kwa sasa anaendelea vizuri

Usisahau kulike and share pia unatupata facebook .  swahili movies .com
pia follow us instagram  swahilimovies

JACK PATRIC YUKO RUMANDE AU KAACHIWA HURU SOMA HAPA

UTATA umeibuka kufuatia kuwepo kwa taarifa kuwa huenda modo maarufu aliyedaiwa kushikiliwa nyuma ya ndondo kwa msala wa madawa ya kulevya nchini China, Jacqueline Patrick ameachiwa huru.

jackPJacqueline Patrick.

 

Utata huo uliibuka mapema wiki hii mara baada ya akaunti ya modo huyo katika mtandao wa Instagram, kuposti picha mpya za Jack hali iliyowafanya wafusi wa mtandao huo kuamini kwamba yupo huru.
“Haiwezekani mtu awe lupango halafu aweze kuingia Instagram na kuweka picha mpya…au kaachiwa huru?” ilihoji mmoja wa wadau wa mtandao huo.
Baada ya komenti hiyo, wafusi wengi mtandaoni waliweza kuamini kuwa aliyeposti picha hizo ni Jack kwani akaunti iliyotumika ni ileile aliyokuwa akitumia modo huyo.JUX1 Jux.

Paparazi wetu naye hakuwa nyuma, alijiridhisha kwa kutazama baadhi ya komenti za kipindi cha nyuma ambazo aliwahi kukomenti katika picha za modo huyo na kuamini kabisa akaunti iliyoposti picha mpya ni Jack.
Wakati tunakwenda mitamboni, mdau mmoja wa burudani alihojiwa na kusema huenda akaunti hiyo ya Jack imetumiwa na msanii wa Bongo Fleva anayefahamika kwa jina la Jux ambaye anatajwa kuwa ni mpenzi wake, alipoulizwa Jux, alisema

jux-4jack na jux  kabla ya matatizo

“Jack yupo fresh kabisa niliongea naye…ila amesafiri…”
Jack alidaiwa kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya Heroin kilo 1.1 Desemba 19, mwaka jana. Hadi leo sakata lake linawafanya watu wabaki gizani wasijue kinachoendelea.

Usisahau kulike and share pia unatupata facebook .  swahili movies .com
pia follow us instagram  swahilimovies