Matusi ya kwenye mitandao ya kijamii yamuumiza Wema Sepetu kwa kumgusa mama yake Mzazi

 

wema7

Wema na Mama yake

Mtandao maarufu wa kijamii wa Instagram umekuwa sehemu ambayo mambo mengi yanafanyika siku hizi na kuwaacha watu wengine wakifurahi, kukasirika na wengine wakitoa machozi kutokana na vita isiyo rasmi inayoendeshwa na team zinazoundwa na mashabiki wanaodai kumlinda mtu fulani maarufu.

Vita ya “team” hizi imekuwa serious zaidi kwa wasanii wa kike na mara nyingi hushambuliana kwa maneno na hata matusi ya nguoni pale mmoja anapotaka kuvuka msitari wa mwingine.

Vita hiyo imemgusa Wema Sepetu na kumuumiza zaidi baada ya kuvuka na kumgusa mama yake mzazi kwa matusi waliyokuwa wakimmiminia Wema.

Kupitia Instagram, Wema ameeleza jinsi alivyoumizwa na matusi  hayo hasa kwa kumuingiza mama yake asiye na hatia katika ugomvi wao.

“Dah…! Sijui hata niseme nini…! Ila si mlitaka kuniumiza… leo mmefanikiwa… nawapeni hongera…. Tena mmetisha haswa… Kila sjku huwa hata siumizwi na matusi yenu cuz naonaga kama ni mnajisumbua tu… Hakuna siku nimelia kwa uchungu kama leo… I min mnitukane mimi mpaka mchoke but leave my mum out of it… Kawakosea nini nyinyi mama angu mpaka mfanye hivyo… Mzazi nwenyewe ndo nimebakia nae mmoja tu… mnataka afe na yeye nibaki yatima sio… dah… leo mmeniweza… saana jamani… Basi naomba isifike huko… nina uchungu sana na mama angu … nampenda sana mama angu ila naona mnataka kuniulia mama angu… Picha halisi ndo hio hapo juu kweli mtu uende ukamfanyie hivyo mama wa mwenzako… una mama wewe.. au uliokotwa na hujui uchungu wa mama… dah… nime surrender leo…. hongera zenu narudia tena… mmeniweza leo…. dah… Mungu nipe nguvu ktk hili jamani… Kwani nilichokikosea haswa ni kitu gani mpaka iwe hivi . Nimekosa nini mimi yarabi toba…. Eeeh mungu… Dah… Ila nashkuru…..”

Nini maoni yako kuhusu mambo kama haya ya uzalilishanaji kwenye mitandao ya kijamii?

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

CREDIT :Bongo movies

Tupe maoni yako hapo Chini..!!

SHEHE Amcharukia Jackline Wolper. Ni kutokana na tabia yake ya kubadili badili dini.

 

 

SHEHE Amcharukia Jackline Wolper. Ni kutokana na tabia yake ya kubadili badili dini.

TABIA ya staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kubadilibadili dini mara kwa mara imeonekana kuwakera watu mbalimbali akiwemo Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum ambaye amemcharukia vikali.

Wolper kiimani ni Mkristo lakini hivi karibuni alibadili na kuwa Muislam kabla ya kurejea tena kwenye imani yake ya awali ya ukristo.

Sababu ya Wolper kubadili dini ilikuwa ni kufunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake Abdallah Mtoro ‘Dalas’, walipoachana akaamua kurudi kwenye ukristo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi juzikati, Shehe Salum, alisema Wolper anapaswa kujichunguza na kubadilika haraka kwani kitendo anachofanya ni kinyume na taratibu za dini.
“Siyo vizuri hata kidogo na hata dini zote zinakemea kitendo cha kuchezeachezea dini kwani ni chukizo kwa Mungu.

“Kwa upande wa Dini ya Kiislamu, kuna sheria kali zaidi kwa mtu akionekana na tabia hiyo, anaweza hata kuuawa hivyo wanaofanya mchezo huo waache kwani siyo vizuri. Huko ni kumfanyia Mungu dhihaka,” alisema Shehe Salum na kuongeza:

“Unajua suala la imani ni kitu kinachomhusu mtu binafsi, ni vyema kufanya uamuzi wa hakika na kushika njia moja na siyo kufanya dhihaka na dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kitu kibaya sana.”
Naye Juma Suleiman, mkazi wa Ilala, jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wetu kuwa, katika imani ya kiislam kunakatazwa watu kucheza na dini huku akisisitiza anayefanya hivyo anaweza kulaaniwa.