huyu ndo boss wa IPTL/ESCROW ambaye anacheza madili na viongozi wa serikali ili kuihujumu nchi yetu pia boss huyu ndiye alisababisha chama cha KANU nchini kenya kuanguka kwenye uchaguzi mkuu baada ya baadhi ya viongozi wa serikali ya KANU kucheza dili na huyu IPTL na kuiingiza mkenge serikali ya kenya.
leo hii amehamia Tanzania anakula dili na vigogo wa serikali kuliangamiza taifa umeme umepanda bei kwa ajili ya nguruwe pori huyu akisaidiana na mamba na viboko walioko serikalini.
inasikitisha na inauma sana pale ambapo umeme ulikatika kwenye miji yote ya tanzania kwa muda wa siku 2 wakati suala hili linaendelea bungeni,wapiga debe,machinga na maskini wengine walichanga pesa sehemu mbalimbali mbeya mjini na tukuyu wakanunua mafuta na kuweka kwenye jenereta ili wawashe tv waone kiama cha wezi wa pesa za escrow lakini cha kusikitisha ni pale wabunge wa ccm wanapoacha majukumu yao na kuanza kuwatetea wezi wa pesa za escrow bila aibu yoyote hakika inauma sana.yani watu wameingiliwa umeme umekatika wanenunua mafuta ili waangalie bunge wabunge wa ccm wanatetea uovu?
ndugu zangu hakika umefika muda wa kufanya maamuzi magumu .
Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more
CREDIT :http://www.tanzaniaclassic.com
POSTED BY : Hamm Chande