Diamond Amwita Jokate mnafki, Amshangaa Kwakutoa Pongezi

 

DIAMOND332
jokate and diamond

Mkali wa ngoma ya Nana,ambaye amenyakua tuzo ya MTV MAMA kama Mtumbuizaji Bora wa Afrika,Diamond Platnamz amemjibu mwanamitindo Jokate Mwegelo baada kuandika ‘status’ kwenye akaunti ya Instagram yake na kumpongeza msanii huyo kunyakua tuzo na kusema mbona hakumsapoti kwa kumpost kwenye akaunti yake kabla ya kutwaa tuzo hiyo.

Akizungumza na XXL ya Clouds Fm,Diamond alisema kuwa baada ya kuambiwa alichopost Jokate kumjibu Diamond baada ya kupost video ikimuonyesha mwanamitindo huyo akicheza ngoma yake ya Mdogomdogo alisema kuwa amecheka na nimesikitishwa kwani huwa anazungumza vitu vingi na yeye amecheza kama ‘fun’ na yeye amempost kama ‘fun’ wake na ile ‘caption’ yake hajamuandika jina ha hajasema chochote kwanini yeye amejishuku hivyo kuna namna nyuma.

’Mbona huwa napost watu wengi tu tena naandika ‘caption’ zangu za vituko vituko mimi ni mswahili nimezaliwa Tandale nimekulia Tandale na Tandale kumenifanya leo niwe hapa nilipo mbona huwa naandika caption za uswahili na hakuna anayejibu ila yeye tu ujue hapo kuna tatizo kwani kuna ubaya gani? Yeye aone tatizo kuandika mimi Mtanyooka tu kama yeye haimuuhusu basi ukiona hivyo kuna kitu kinamuhusu,’’alisema Diamond.

‘’Nikasikia kuwa kasema kuwa ndiyo maana wanaogopa kusapoti wasanii wa Tanzania kwa sababu wakisapoti wanadhalilishwa yeye mpaka naenda kuchukua tuzo ya Mtumbuizaji Bora yeye amenisapoti nini hajawahi kunipost hata tuzo moja sasa hivi ndiyo anajishaua eti ananipa hongera kwa tuzo ningemuona wa maana angepost watu wapige kura na kuwahamasisha ili ushindi urudi nyumbani lakini kwa chuki alizojazwa pasipo na sababu na roho mbaya aliyowekwa na watu imemfanya ashindwe kunipost na kutengeneza chiki za chinichini wakidhani wakiwapigia kura Wanageria mimi nitakosa tuzo Mungu amewalaani mimi nimeshinda halafu anajifanya anatoa hongera eti wanasapoti muziki wa Tanzania au kwasababu wameona tuzo imekuja ndiyo wanajifanya wanatoa hongera tuache unafiki,’’alimalizia Diamond.

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

CREDIT : Here

Tupe maoni yako hapo Chini..!!

Asante kwa wanaonikubali na wasionikubali wasubiri tu lazima watanikubali:Muigizaji Claurice safi

Asante Sana kwa wanaonikubali,na wasiyo nikubali wasubiri, nitawaleteya mazuri adi watanikubali.  Katika kipindi cha hivi karibuni Muigizaji Claurice safi ni mmoja kati ya waigizaji wakuu wa Tamthilia ya Mawenge  ameonekana akiafanya vizuri na akiwa amebeba nafasi kubwa katika tamthilia hiyo , licha ya kuwa alishacheza filamu mbalimbali katika kundi hilo la VAD lakiniwengi walikuwa hawamfahamu  mpaka katika tamthilia hii ya mawenge ambayo amecheza muuhusika mkuu ,

                            Mbali na uwezo wake mkubwa wa kuigiza katika tamthilia hiyo ambayo anaigiza kama mwanamke kipofu anaenyanyaswa na mme wake , mashabiki wengi wangependa kumjua kiundani  kuhusu muigizaji huyu ndipo swahili movies tulipoamua kumtafuta na kufanya nae mahojiano fatilia hapo chini uweze kujua mengi kuhusu Muigizaji huyu matata kutoka kampuni yako kongwe  V.A.D Film Production  ya Denmark.

11768698_980557302007831_117199046_o

Mashabiki wanaona kazi zako nzuri na uwezo wako mkubwa katika uigizaji lakini hawajui jina lako halisi ni na umeanza lini shughuli hizi za uigizaji ?

Mimi majina yangu, yakuzaliwa ni safi Clarice Bernard.  kazi yangu ya uigizaji nilianza toka mwaka2007 kwenye kikundi kimoja kilikuwa kinaitwa one love Kilichokuwa kusini mwa kongo UVIRA .

Kitu gani kimekuvutia kuingia katika Uigizaji ?

mimi kitu ambacho kilinivutiyaga zaidi kwenye uhigizaji ni nafsi yangu yenyewe kwanza, sababu kipindi nilikuwa mtoto nilianza kuigiza kanisani, piya na shuleni.nakipindi tamthilia zilianza kuchezwa,tanzania ndipo nilivutiwaga Sana nikasema lazima na mimi siku moja nije kuwa muigizaji, kipindi  icho KIDEDEA, na MAMMBO HAYO walikuwa wamepamba moto.

Umeshafanya filamu au kazi ngapi  Mpaka sasa waweza zitaja?

Nimesha fanya filamu zaidi ya saba nimefanya filamu nne Congo,1 one buy one ,Tueshimu wazazi, love, mapenzi ayachagui.kwa apa Denamrk nimecheza filamu, 3 sorry my wife, maisha ya ndotoni, na nimwamini nani?. Ila bado zipo zinafanyiwa editing, zipo njiani zinakuja.

2014-04-03-21.20.49

 Wewe na mme wako wote ni waigizaji katika kampuni moja je kuna matatizo yoyote mnayokumbana nayo mkiwa wote ni familia moja yanayotokana na sanaa ? pia siku chache zilizopita ilijifungua mtoto na kuna matatizo au changamoto zozote unazopata ukiwa shooting kama msanii na una mtoto mdogo labda kulia ?

Matatizo hayawezi yakakosa tukiwa tupo kazini. Ila siyo mara kwa Mara.Namshukuru mungu sababu mwanangu siyo mlizi Sana, uwa hasumbui kipindi cha shooting, ilo nasema Asante kwa mungu.

Nini mipango yako ya badae katika sanaaa  na  Kwa africa ni msanii gani mkubwa unaependa siku moja uje uigize nae ?

Namuomba mungu asaidie kikundi chetu cha V.A.D kiendelee zaidi na zaidi. Kingine napenda niwe muigizaji zaidi ya hapa nilipo.

Wasanii hote ambaho wanakipaji Chao, mimi siku moja natamani kuigiza nao.Kama nilivyo igiza na Lucy komba nimefurahi Sana nimejifunza mengi kutoka kwake.

Unaushauri gani kwa wasanii wenzako  na kwa mashabiki wako ?

 Wasanii Tuwe tu na upendo wa kweli, usiyo na chuki kwa ndani, na tuwe tunaungana mkono .wale ambao wametowa kazi,tuwe tunawasapoti, asante sana kwa mashabiki wangu wale wanaonikubali,na wasiyo nikubali wasubiri, nitawaleteya mazuri adi watanikubali.

MUIGIZAJI SAFI AKIWA KWENYE PICHA ZA POZI MBALIMBALI

11774362_980557265341168_1637793542_n

 

11753808_980557342007827_2040352622_n

11774368_980557305341164_1136168413_n

Hizi ni baadhi ya picha za behind the scene za tamthilia ya Mawenge

11225898_10206637581648876_487507409_n

 

11013020_462855743873124_2033451985411260651_n

Selembe Toko akiwa on set na muigizaji claurice

1908156_462855660539799_3654594855329170983_n

https://www.youtube.com/watch?v=kyCnCAU2nJE&feature=youtu.be

Follow us on instagram swahili movies and Like our facebook pages Swahili movies.com and  for more updates about Swahili movies latest news, Scandal, Celebrities, features,european news, American,Australian ,Africa news, Music , news and more

CREDIT : Here

Tupe maoni yako hapo Chini..!!