Yaliyojiri katika ibada ya kumuombea Kanumba, Wasanii wasema haya Soma Hapa

Akizungumza na gazeti la Mwananchi Leo, Mama Kanumba amesema, ujio wa wasanii maarufu wachache kwenye ibada ya kumbukumbu ya Steven Kanumba unaonyesha kuwa wao wameshamaliza msiba, lakini kwake yeye msiba bado upo.
.
“Idadi ya wasanii maarufu waliokuja hapa ni wachache ukilinganisha na namna Kanumba alivyoishi nao, lakini ndio hivyo huwezi kuwalazimisha na isitoshe wao labda wanaona wamemaliza msiba lakini Kwangu bado upo Ila ninachowaombea yasije yakawakuta kama haya ndio watajua nini namaanisha” amesema Mama Kanumba
.
Aidha, amewashauri wasanii kuwa na upendo kama walivyokuwa wakihusiwa na Marehemu Kanumba

Source: MWANANCHI

Leo April 07, 2018 ni maadhimisho ya miaka sita tangu alipofariki msanii wa filamu Bongo, Steven Kanumba ambapo ibada ya kumuombea ilifanyika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Baadhi ya wasanii wamejitokeza katika siku hiyo muhimu, Mama Mzazi wa Kanumba pamoja na Paster Miyamba mmoja wa wasanii maarufu aliyeshiriki ibada hiyo. Angalia Picha hapa chini



xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
https://www.youtube.com/watch?v=_NaWOSR1kR8
https://www.youtube.com/watch?v=eNIp3tDBKLg