MAMA :UMAARUFU WA MOBETO NILIUONA MAPEMA


MAMA wa mwanamitindo mwenye jina kubwa Bongo, Hamisa Mobeto, Shufaa Rutiginga ‘Mama Mobeto’, ameibuka na kusema kuwa aliuona umaarufu wa mwanaye mapema tangu alipokuwa na umri mdogo. Akizungumza na Risasi Jumamosi, mama huyo alisema kuwa, mwanaye alionesha mapema atakuwa mtu f’lani kutokana na jinsi alivyokuwa akijiweka na watu wengi walimwambia kuwa atakuwa mlimbwende. “Unajua Mobeto alikuwa akijipenda tangu mdogo na alikuwa na mambo f’lani ambayo niliamini akikua atakuwa mtu f’lani mwenye jina mjini,” alisema mama Mobeto.
Mama huyo aliendelea kusema kuwa, baada ya kuona umaarufu wa mwanaye alijitahidi kumpa malezi mazuri na makini kwani alimlea peke yake bila kuwa na baba. “Baba wa Mobeto (Hassan Mobeto) alifariki dunia mapema sana hivyo nilimlea peke yangu na ni mwanangu wa pekee, nashukuru kuona anakua vizuri,” alisema mama Mobeto
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
https://www.youtube.com/watch?v=Tqy4ziXjh6U&t=107s